Tumgik
#wanaume
rwizakakiza · 24 days
Text
Somo: MAJIRA NA NYAKATI ZIMEBEBA MAISHA YAKO. (Part 15: MAAMUZI YA MWANA...
youtube
Somo: MAJIRA NA NYAKATI ZIMEBEBA MAISHA YAKO
°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°
Fuatilia YouTube.
Https://youtube.com/@Rwizakakiza
Sehemu 15:
‭""Kwa KILA JAMBO kuna MAJIRA yake, Na WAKATI kwa KILA KUSUDI chini ya mbingu""
.....Mhubiri 3:1.....
6. AINA 2 ZA MAJIRA NA NYAKATI KATIKA MAISHA YAKO.
6. 1. MAJIRA NA NYAKATI YA MWANADAMU.
Haya ni majira na nyakati zinazopangwa na Mwanadamu kwa utashi, uwezo, Ugunduzi na mamlaka aliyopewa na MUNGU. Ni uwezo wa kutambua majira na nyakati na namna ya kuenenda kwa nyakati zenyewe ili kuendesha maisha yake ya kila siku na maisha ya mwingine pia.
Mwanadamu huyu katika majira yake na nyakati zake za kibinadamu anaweza kupanga aishije (vibaya au vyema). Kutokana na anavyopanga kuishi anaweza kusaidia mapenzi ya MUNGU kutumia au akakwamisha mapenzi (makusudi) ya MUNGU yasitimie kwa muda sahihi.
Tujifunze jambo kwa Bikira Maria na Nabii Eliya.
(i). BIKIRA MARIA.
.....‭ Malaika akaingia nyumbani kwa Bikira Mariamu akasema, "Salamu, uliyepewa neema, BWANA yu pamoja nawe". "Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa MUNGU". "Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita YESU".
Mariamu akamuuliza malaika, "Litakuwaje neno hili, maana sijui mume?"
Malaika akajibu akamwambia, "ROHO MTAKATIFU atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa KITAKATIFU, Mwana wa MUNGU". kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa MUNGU".
Mariamu akasema, "Tazama, mimi ni mjakazi wa BWANA; na iwe kwangu kama ulivyosema". Kisha malaika akaondoka akaenda zake.
.....Luka 1:28 - 38......
Hapo unaona Mariamu alikuwa tayari ameposwa, kwa lugha nyingine alikuwa na MIPANGO au makusudi yake kimaisha ataishije, na inaonekana yupo kwenye maandalizi ya kuolewa akiwa amejitunza (tofauti na mabinti wa sasa wanaishi na wanaume kabla ya ndoa takatifu). Lakini katikati ya maandalizi MUNGU anampa majira na nyakati zake Kwanini Mariamu alimuumba. Ashukuriwe MUNGU Mariamu alikubali.
Bikira Maria alikuwa na uwezo wa kukataa ndio maana MUNGU hakumvamia Mariamu alafu ajikute ana mimba, alielezwa na Mariamu akakubali kutekeleza majira na nyakati za MUNGU.
(ii). NABII ELIYA.
.....Yezebeli akampelekea Eliya mjumbe, kusema, "Miungu wanifanyie hivyo na kuzidi, nisipokufanya roho yako kesho, panapo wakati huu, kama roho ya mmojawapo wa hao (Manabii).
Eliya akakimbia, akaendelea katika jangwa mwendo wa siku moja, akaenda akaketi chini ya mretemu. AKAJIOMBEA ROHO YAKE AFE, akasema, Yatosha; sasa, Ee BWANA, uiondoe roho yangu; kwa kuwa mimi si mwema kuliko baba zangu"
BWANA akamwambia, Enenda, urudi njia ya jangwa la Dameski; UKIFIKA , MTIE MAFUTA ELISHA mwana wa Shafati wa Abel-Mehola mtie AWE NABII MAHALI PAKO.
.....1Wafalme 19:2 - 16....
Eliya pamoja na utumishi uliotukuka alioufanya makusudi ya MUNGU hayakutimia kupitia yeye, alikwamisha Majira na nyakati za MUNGU kwa hofu ya kumwogopa Yezebel.
Je wewe unaruhusu mapenzi ya MUNGU yatendeke au wewe ni chanzo cha kukwamisha makusudi ya MUNGU yasifanyike kwa muda sahihi?.
ZINGATIO.
Mwanadamu anapotumia vibaya majira na nyakati zake, anakwamisha kusudi la MUNGU lisitimie kwa wakati. Pili anakuwa chanzo cha kuleta au kusababisha majira na nyakati za taabu na mateso kwa wengine au hata kwake mwenyewe.
Mfano.
BWANA YESU anasema
....."MSIWAOGOPE WAUUAO MWILI, WASIWEZE KUIUA na ROHO; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum".
......Mathayo 10:28.....
Kwa lugha hiyo sio kila kifo ni mpango wa MUNGU, ila kuna vifo vingine ni MIPANGO ya wanadamu. Maana anasema Usiogope mtu anayeua mwili, mwenye uwezo wa kuua Roho ni MUNGU pekee, lakini tukubaliane watu au mtu ana uwezo wa kukutenganisha mwili wako na Roho yako yaani kwa kukuua kabisa kimwili.
Hivyo mwanadamu ana uwezo wa kuharibu majira na nyakati zake mwenyewe (kwa kujiua /madawa ya kulevya na Ulevi /Uzinzi /ushoga, nk) au kuharibu majira na nyakati za mtu mwingine (kwa kumwaribia maisha /kusingizia /Ubakaji /ulawiti /kulipiza visasi /Chuki, nk).
Lakini pia majira na nyakati zako unaweza kuzifanya zikawa za furaha, amani na upendo na wengine pia wakafurahia majira na nyakati zao kwa sababu yako na mpango wa MUNGU ukawa rahisi kutimia kwako na kwao.
Je majira na nyakati zako na wengine ni zipi?.
6. 2. MAJIRA NA NYAKATI YA MUNGU
....Tutaendelea....
Rejea
“I assure you and most solemnly say to you, whatever you bind [forbid, declare to be improper and unlawful] on earth shall have [already] been bound in heaven, and whatever you loose [permit, declare lawful] on earth shall have [already] been loosed in heaven".
......Matthew 18:18.....
Ev. Erasmus Pascrates Kakiza
+255 782 546 914
@2024 The year of my shining.
0 notes
news2024news · 1 month
Text
Tumblr media
Tanzanian DJ Ally B Tells Women Not to Dump Husbands Who Cheat: "Wanaume Tumeumbwa Hatujakalilika" http://dlvr.it/TBvlkY
0 notes
bongosinematv · 1 year
Video
Mwanamke mlevi aliyebakwa na wanaume 30.
1 note · View note
sariaisrael · 1 year
Text
MWANAMKE WA KWANZA KUWA KOCHA WA TIMU YA WANAUME
Kabla ya kuwa kocha mkuu wa muda wa Forest Green Rovers mwanamke huyo alikuwa bosi wa Akademi ya klabu hiyo….. WALIANZA Waamuzi wanawake wa mchezo wa soka. Wakapewa nafasi kupuliza filimbi katikati ya dimba na wengine wakawa Waamuzi wasaidizi.  Waamuzi wanawake wamepiga hatua katika soka na hawajaachwa nyuma. Chelsea waliwahi kuwa na daktari mwanamke, ambaye alivunja vikwazo vyote vya wanawake…
Tumblr media
View On WordPress
0 notes
ju-st-sam · 1 year
Text
Wanaume ni colorblind lakini wanajua kudifferentiate wasichana weupe na weusi
0 notes
nickhealthcare · 2 years
Text
…Kama wewe ni mwanamke na unatabia kama za #zuwena wa @diamondplatnumz
...Yaani unywaji wa pombe kupitiliza, kushiriki tendo na wanaume wengi, kujichubua n.k!
Ukae ukijua kabisa unajiweka katika hatari kubwa sana yakupata...
1. Maambukizi katika Via Vya Uzazi, kutokana na kuwa na wanaume wengi
2. Kuwahi kuzeeka, kutokana na unywaji wa vilevi kupita kiasi
3. Matatizo ya maini na mafigo kutokana na upakiaji wa sumu nyingi mwilini zitonazo na vilevi
4. Matatizo ya ngozi, ngozi Kupoteza uhalisia wake kutonana na sumu nyingi mwilini na matumizi ya vipodozi vikali n.k
...Hayo ni mambo baadhi ambayo nimeyaorodhesha kwa mwanamke mwenye tabia kama za #zuwena
Lakini habari njema ni kwamba kama wewe ni muhanga wa changamoto Moja au zaidi au ambayo sijaiorodhesha hapo juu...
@nickhealthcare ndo suluhisho la changamoto zako wasiliana nasi kupitia nambari za simu za
☎️+255692438154
𝐍𝐈𝐂𝐊𝐇𝐄𝐀𝐋𝐓𝐇𝐂𝐀𝐑𝐄:-
"𝐓𝐔𝐏𝐄 𝐈𝐌𝐀𝐍𝐈 𝐍𝐀 𝐔𝐀𝐌𝐈𝐍𝐈𝐅𝐔,
𝐓𝐔𝐓𝐀𝐊𝐔𝐏𝐀 𝐅𝐔𝐑𝐀𝐇𝐀 𝐍𝐀 𝐀𝐅𝐘𝐀".
▪︎
▪︎
▪︎
#tanzania🇹🇿 #nickhealthcare #MaishaNiAfya #Afya #who #furaha #fahamuzaidi #elimu #sanaaimezaliwaupya #hiiniyetusote #swahili #huunimwakawako #healthy #healthlifestyle #0692438154
Tumblr media
1 note · View note
drkangile · 2 years
Photo
Tumblr media
❤️> Ndoto Ya Kila mmoja ni Kua na Muonekano Mzuri Na Sio tu Wa Kimavazi Hata Muonekano Wa Mwili Wake Kwa Ujumla ...... .... Ila Hali Ya Kua Kibonge , Kua Kitambi hua Inakera Sana ... .. Hata unapokua unajaribu Kwenda Mtoko Na Marafiki Zako unatumia Muda Mwingi Kujiaanda .......😝 ... Kwa Sababu Kila Nguo Aliyokua Anavaa Sio Tu Kwamba Haikutoshi Vizuri Ila Haupendizi Kabisa..... 😁 .... Bahati unaanza Kufuatilia Video Mbalimbali Mtandaoni Kuhusu Kupunguza Uzito...... ..Ukanunua Vifaa vyote Muhimu Vya Mazoezi ... ...Ulianza Kukimbia Jogging Pia .... Ulikua na Usongo Wa Kupungua Kwa Hiyo Hakuishia Hapo Alibadilisha Zaidi Ya Aina Nne Ya Diety Lakini Wapi ......😁😢 Badala Ya Kupungua ulijikuta Anakonda ...au hupungui kabisa 🚶‍♂️🚶🏾‍♀️ .... PengineHukufahamu Kua Kupungua Haku Hitaji Mazoezi Pekee Au Kujinyima Kula .... Mfano: Ili Kupungua Kirahisi Nje Ya Diety Au Kufanya Mazoez Ni Lazima Usafishe Mfumo Mzima Wa Mwili ...... ... Kwa Kuondoa Sumu Ambazo Tunazipata Kutokana na Vyakula Tunavyokula ..... Hata Hewa Tunayovuta........ Na Ndio Maana unapokutana Na Sisi utatumia Wiki Moja tu Kuanza Kuona Matokeo Na...Mwezi Mmoja tu Kupata Muonekano Aliokua Anahitaji Iko Hivi Kupungua Ni Ujuzi ......... ... Inawezekana Umewai Kujaribu Kutumia Njia Mbambali Kama Bahati Za Kupunguza Uzito Na Kitambi Bila Mafanikio ....... 😢😢 Tuna Kuelewa Sana Jinsi Unavyo Jinsi Na Unavyo Pambana Kua Bora ..... ... Uzoefu WETU wa Zaidi Ya Miaka 21 Katika Kuwasaidia Wanaume na Wanawake Kupungua .... Kwa Bahati Mbaya Zaidi Hatusaidii Kila Mtu, Ila Kwa Watu Wachache tu Walio Serious.... Hivyo Kama Unatamani Kupata Program Na Ushauri Wa Jinsi Ya Kupunguza Uzito Na Kitambi Ndani Ya Muda Mfupi..... Basi karibu Tuzungumze Au Tupigie Moja Kwa No. 0717174151 https://www.instagram.com/p/CoEdrwRNAsr/?igshid=NGJjMDIxMWI=
0 notes
rwizakakiza · 5 months
Text
Somo: USIMWACHE MUNGU.
°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°°
Fuatilia YouTube.
Https://youtube.com/@Rwizakakiza
Sehemu .I.
UTANGULIZI.
Nini maana ya KUMWACHA MUNGU?
>Ni hali ya kutengana na MUNGU, kutotii Neno lake na kutoyapa kipaombele mambo yote yanayomuhusu MUNGU.
>Ni hali ya kutengana na YESU KRISTO ambaye ni Ufunuo wa MUNGU mwenyewe, Maana huwezi kumjua na kumfahamu MUNGU aliye hai, pasipo kufunuliwa na YESU KRISTO aliye Njia, Kweli na Uzima.
.......YESU akamwambia, "Mimi ndimi NJIA, na KWELI, na UZIMA; mtu haji kwa BABA, ila kwa njia ya mimi. Kama MNGALINIJUA MIMI, mngalimjua na BABA; tangu sasa mnamjua, tena MMEMWONA". Filipo akamwambia, 'BWANA, utuonyeshe BABA, yatutosha'. YESU akamwambia, "Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? ALIYENIONA MIMI AMEMWONA BABA; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba?"
.....Yohana 14:6-9.....
Hakuna njia ya kumfahamu MUNGU wa kweli pasipo YESU KRISTO, la sivyo utakuwa unamtafuta MUNGU kwa kupapasa papasa na itakuwa vigumu kumjua na ikiwa vigumu kumjua MUNGU, sio rahisi Kumpenda, na usipompenda utaachama naye au utatumikia vitu vingine na kuviabudu ukifikiri unamtumikia MUNGU.
Sauli akiwa hajakutana na BWANA YESU aliua watu wengi akifikiri anampendeza MUNGU, Ukweli alikuwa gizani na alijitenga na MUNGU mbali.
.....Sauli alikuwa AKIONA VEMA kwa kuuawa kwa Stefano. Sauli AKALIHARIBU KANISA, akiingia kila nyumba, na kuwaburuta wanaume na wanawake na kuwatupa gerezani. Sauli, AKIZIDI KUTISHA na KUWAZA KUWAUA wanafunzi wa BWANA, AKAMWENDEA Kuhani Mkuu, AKATAKA ampe barua za kuenda Dameski zilizoandikwa kwa masinagogi, ili AKIONA watu wa NJIA HII (Wakristo), waume kwa wake, awafunge na kuwaleta Yerusalemu.
.....Mdo 7:60, 8:3, 9:1-2...
Kwake kuua na kutesa watu alikuwa anajua anampendeza kabisa MUNGU, lakini hakujua kama ametengana naye muda mrefu na anachokifanya anamuudhi MUNGU.
.....Sauli alipokuwa akisafiri; Ghafla ikamwangaza kote kote Nuru kutoka mbinguni. Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, "Sauli, Sauli, mbona waniudhi?" Sauli akauliza, 'U nani wewe, Bwana?' YESU akasema, "Mimi ndimi YESU unayeniudhi wewe".
......Mdo 9:3-5......
Je wewe unamuudhi MUNGU?
......Tutaendelea......
Rejea
‭‭ "Now get up and go into the city, and you will be told what you must do.”
......Acts 9:6......
Ev. Erasmus Pascrates Kakiza
(WhatsApp: +255 782 546 914)
@2024 The year of my shining.
0 notes
swahili-bible · 2 years
Text
1. BIBLIA: UJUMBE WA MUNGU KWA MWANADAMU
“Neno lako ndio kweli”
Shabaha
Ni kuonyesha kwamba Biblia ni neno la Mungu.
Muhtasari
Biblia ni muujiza uliomo katika mikono yetu. Ni kitabu kinakuelezea habali za mabo yaliyo pita bali pia kina kinaunabii mwingi sana, ikiwa na maana kwamba kinatuambia mambo yajayo, mambo ambayo vitabu vingine vyote haviwezi kutujulisha.Kina tufundisha yale yote yaliyo muhimu kwetu kuyajua kuhusu Mungu, mambo yake ambayo Mungu aliyafanya wakati uliopita, anafanya nini kwa wakati huu na kwa wakati ujao amekusudia kufanya nini. Biblia pia hutuonyesha namna itupavyo kuishi ili kumpendeza Mungu. 2 Timotheo 3:14-17, 2 Petro 1:19-21.
BIBLIA
Neno “Biblia” maana yake ni “kitabu”. Neno “takatifu” maana yake “tenga” au “weka kando”. Kwa hiyo Biblia takatifu ni kitabu kilichotengwa kutoka vitabu vingine. Mungu amekitenga kuwa kitabu pekee kinacho eleza Kweli kuhusu Mungu na mipango yake kwa wanadamu. Tunapoifungua ni kweli kuwa ni mkusanyiko wa vitabu sitini na sita vilivyounganishwa kuwa kitabu kimoja. Biblia imegawanyika sehemu mbili. Agano la kale na Agano jipya.
Agano la kale lina vitabu 39. Musa ndiye mtu wa kwanza kuandika vitabu vitano yapata kama miaka 1500 kabla ya Kristo kuzaliwa. Kitabu cha mwisho kati ya vitabu vya Agano la Kale kiliandikwa na nabii Malaki yapata kama miaka 1000 baadaye.
Agano Jipya lina vitabu 27. Lina tueleza kuhusu maisha na kazi za Yesu Kristo na jinsi wanafunzi wake walivyoeneza habari njema kuhusu Yesu Kristo na Kuja kwa fufalme wake duniani kote. Sehemu hii ya Biblia iliandikwa wakati wa Mwanzo wa miaka miamoja baada ya Yesu kuzaliwa. Jifunze majina ya vitabu vya Biblia kwa moyo. Itakusaidia katika kusoma na kujifunza kwako Biblia kila siku. Tumeona kwamba Biblia iliandikwa zaidi ya miaka mingi, yapata kama miaka 1600 katika kukamilisha kwake; na bado waandishi wote wanaeleza habari za aina moja zinazo pendeza na kustaabisha. Wanatujulisha kwa namna iliyotofauti, makusudi makubwa kwa ajili ya dunia hii na kwa ajili ya mwanadamu anayekaa juu yake.
JINSI BIBLIA ILIVYOANDIKWA
Ni kwa jinsi gani Biblia, ambayo iliandikwa zaidi ya kipindi cha muda mrefu sana tena kwa kuandikwa na watu wengi tofauti na walioishi sehemu tofauti, wote waelezee ujumbe mhimu wa aina moja? Mtume Petro anatuambia kwamba: “Watu wa Mungu walinena wakiongozwa na Roho Mtakatifu” (2 Petro 1:21). Ilikuwa ni nguvu takatifu za Mungu iliyowapatia watu hao fikra katika mawazo yao nao wakayanena yale ambayo ni mawazo ya Mungu, kwa hiyo, ingawaje watu wengi waliandika Biblia, lakini Mungu mwenyewe ndiye mtungaji wa Biblia.
KWA NINI BIBLIA ILIANDIKWA
Katika Biblia tunaambiwa yote ambayo ni ya muhimu kwetu kuhusu Mungu na mpango wake kwa dunia na wanadamu wanaokaa juu yake. Mungu anataka sisi tumjue na tumpende Yeye. Kuna aina nyingi ya habari nzuri zinazovutia na kufurahisha katika Biblia kuhusu wanaume na wanawake waaminifu waliompenda na kumtii Mungu. Habari hizi zinatusaidia sisi kujifunza kuwa waaminifu na watiifu pia. Kwa hiyo kwa kadri tunavyosoma Biblia, na ndivyo kadri tunavyompenda Mungu na kujaribu kumpendeza Yeye. Na nia zetu zitaweza kuwa nia yake Mungu na njia zetu zitabadilishwa kufunana na njia zake.
KUSUDI LA MUNGU LA WAKATI UJAO KWA DUNIA
Kusudi la Mungu ni kuijaza dunia utukufu wake Mungu. “Hakika kama niishivo, dunia yote itajazwa na utukufu wa Mungu” (Hesabu 14:21). Ilikufanya hili atamtuma Yesu Kristo kurudi hapa duniani kuuweka ufalme wa Mungu hapa duniani (Matendo 1:10–11, Dan 2:44). Kwanza atawafufua wafu wale waliojua kweli na atawapatia wote uzima wa milele waliompenda na kumtii. Kisha watamsaidia kuifundisha dunia njia ya haki ya Mungu. Atawaangamiza wabaya na kutawala katika Yerusalemuakiwa Mfalme wa dunia yote. Kisha kwa miaka elfu moja Kristo na watakatifu wake wataibadilisha dunia kuwa mahali ambapo viumbe vyote vitampatia Mungu utukufu na sifa milele.
YANAYOFUNDISHWA NA BIBLIA KUHUSU MUNGU.
Biblia inatuambia kuwa Mungu:-
Kwamba Mungu ni Roho au kamwe Yeye hafi
Kwamba kuna Mungu mmoja (Kumb. 6:4), Muumbaji wa vitu vyote.
Kuwa Mungu ni mwema na mvumilivu na huwa saidia na kuwaongoza wale wanaomwanini yeye. Pia yeye ni mwenye haki na mwaminifu atawahukumu waovu waliomkataa Yeye pamoja na njia zake.
Kuwa Roho Mtakatifu nguvu za Mungu ambayo kwa njia yake Mungu hutenda matendo yake makuu na ya ajabu.
Kwamba malaika ni watumwa wake wa kiroho au wajumbe wake watendao mapenzi yake.
FUNDISHO
Katika Biblia tunajifunza yale ambayo Mungu anataka sisi tuyafanye. Kuna ambo ambayo tunapaswa kuyafanya na mambo yale ambayo hatutakiwi kuyafanya. Wale watu wanaofanya yale Mungu anayoyataka kwa sababu wanampenda na kumwamini, siku moja watapewa uzima wa milele katika ufalme wa Mungu. Hakuna sehemu nyingine isipokuwa katika Biblia ndipo tunakuta njia ya uzima wa milele na furaha tele. Tunatakiwa tusome biblia kila siku naye Mungu atatuongoza katika maisha yetu yote. “Neno lako ni taa ya miguu yangu na mwanga wa njia yangu” (Zaburi 119:105).
MAELEZO YA NYONGEZA
Unabii ni nini? Wakati ambapo watakatifu wa Mungu walipotabiri, walinena habari ya mambo yajayo. Kwa mawazo yetu sisi hatuwezi kuyasema yale yatakayotokea wakati ujao ila Mungu ndiye anaweza kusema yatakayotokea wakati ujao. Biblia ina mkusanyiko mwingi sana wa unabii. Zingine zimekwisha kutimia kwa kila namna ya maelezo yaliyokuwa yametabiriwa kiasi ambacho tunakuwa kuamini kwa uhakika kwamba hata unabii mwingi ambao haujatimia bado, utatimizwa kwa kweli hakika. unabii mwingi sana wa Biblia unaonyesha waziwazi kwamba yesu kristo atarudi duniani, na zinaeleza ishara zitakazo kuwepo kabla hajarudi.
Fikiria baadhi ya ishara hizi:
Kutakuwepo na dhiki kuu na vita kati ya mataifa ya dunia (Dan 12:1, Luka 21:25 – 26.)
na dhambi zitaongezeka duniani (Mathayo 24:37 – 39).
Watoto hawatawaheshimu wazazi na wakubwa wao, na watu watapenda anasa kuliko kumpenda Mungu (2 Timotheo 3:1-5).
nchi ya Urusi itakuwa ni nchi yenye nguvu sana na itataka kuitawala dunia (Ezekieli 38).
Wayahudi watarudi katika nchi yao wenyewe (Eze 38:8, 12).
Unabii huu unaendelea kutimizwa siku hizi machoni petu wenyewe na huu ni ushuhuda kwamba Biblia ni neno la Mungu hakika, na ya kuwa siku ile ikaribu sana ambapo Mungu atamtuma Yesu Kristo kurudi duniani kuuweka ufalme wa Mungu.
MASWALI
Maisha ni Mafupi
Ni nani mwandishi wa Biblia?
Biblia Takatifu maana ninini?
Kuna vitabu vingapi katika Biblia?
Ni kwa nini Mungu alitaka Biblia iandikwe?
Ni nini makusudi ya Mungu kwa dunia?
Nini maana ya Roho Mtakatifu?
Malaika ni nani?
Makusudi ya Mungu kwa wale wampendao ni nini?
Majibu ya Kina
Biblia inatufundisha nini kuhusu Mungu?
Eleza yale unayoyajua kuhusu mpango Mungu kwa dunia
Majibu ya Nyongeza
Biblia ina unabii mwingi sana unaoonyesha kwamba kurudi kwa Yesu Kristo duniani kumekaribia.
Baadhi ya unabii huu ni nini?
1 note · View note
zephilinecom · 2 years
Text
KIBAMIA (14)
Jina: KIBAMIA Mwandishi: Geofrey Malwa SEHEMU YA KUMI NA NNE ILIPOISHIA... Unajua baadhi ya wanaume huwa wanaona wakipampu haraka ndio wanamkuna vyema mwanamke pindi waingizapo dudu zao lakini sio kweli,mwanamke anatakiwa akuongoze kwa hisia zake,wewe n
Jina: KIBAMIAMwandishi: Geofrey Malwa SEHEMU YA KUMI NA NNEILIPOISHIA… Unajua baadhi ya wanaume huwa wanaona wakipampu haraka ndio wanamkuna vyema mwanamke pindi waingizapo dudu zao lakini sio kweli,mwanamke anatakiwa akuongoze kwa hisia zake,wewe ndio unakuwa unamfuata kwa nyuma,wanawake wote wanapenda pindi unapoingiza dudu uwaanza taratibu kama hutaka vile,jinsi utamu unapokolea ndio kasi…
Tumblr media
View On WordPress
0 notes
msa-firi · 2 years
Photo
Tumblr media
Wanawake wameumbwa na mungu. Wanaume ni ka tumeumbwa na shida. Mtuangu unajua nini baya kuliko kukuwa muuaji, si ni pretending. Huku tao ukiwa msee hauna connection unaeza hata kosa ukedi. https://www.instagram.com/p/CmL-_Q4K_HJ/?igshid=NGJjMDIxMWI=
0 notes
yetusote · 2 years
Text
Tumblr media
2 notes · View notes
enockmaregesi · 5 years
Photo
Tumblr media
Nimeishi na watu kutoka katika mabara yote ya dunia hii. Wanaume wana asili yao na wanawake wana asili yao. Ndiyo maana katika upendo wa PHILADELPHIA, upendo wa wanachama wa mashirika ya siri, wanaume na wanawake hawachangamani. #upendo #love #philadelphia #philadelphialove #secretsocieties #asili #nature #wanawake #women #wanaume #men https://www.instagram.com/p/Bw7BjSOnvzu/?utm_source=ig_tumblr_share&igshid=1ks1y9jwd5n6c
0 notes
afrojuke · 4 years
Text
TMK Wanaume – Wanaume Kazini (MP3 Download)
https://ift.tt/39fxZzv
TMK Wanaume household is a neighborhood that hails from Temeke, Daresalaam, Tanzania. The neighborhood was before all the pieces a combination of three assorted groups that were doing completely on the Tanzanian tune scene. RELATED: Wanaume TMK – Kichwa Kinauma Ft Aslay It’s a mark new day and we’re at ease to bring you a mark […]
AfroJuke - Download Mp3, Latest Naija Music, Latest Bongo flava, South African, Ghana Music & More!
from AfroJuke https://ift.tt/3qRMBen
0 notes
drkangile · 2 years
Photo
Tumblr media
*XPOWER MAN EXTRA CAPSULES* Ni kirutubisho maalumu kwa waathirika wa Punyeto na wenye Upungufu Wa Nguvu Za Kiume. *kirutubisho hiki hufanya kazi zifuatazo:-* ✅Huongeza Hamu Na Uwezo Wa Kufanya Tendo La Ndoa ✅Hufungua Mirija Midogomidogo Ya kibofu Kwenye Uume Ambayo Hufa Kwa Ajiri Ya Umri Na Kisukari/Presha ✅Huondoa Uchovu ✅Huongeza Wingi Wa Afya Wa Mbegu Za Kiume ✅Huondoa Tatizo La Maumivu Uume Ukiwa Umesimama ✅Humfanya Mwanaume Akae Muda Mrefu Kwenye Tendo ✅Huongeza Kinga Kwenye Via Vya Uzazi ✅Humfanya Mwanaume Arudie Tendo Bila Kuchoka Na Kwenye Ubora Wa Hali Ya Juu ✅Huondoa Tatizo La Uume Kusimama Ukiwa Legelege ✅Huondoa Tatizo La Uume Kurudi Ndani Na Kuwa Kama Wa Mtoto ✅Huondoa Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za kiume Na Ugumba Kwa Wanaume. Inbox au #PIGA 0717174151 (at Dar es Salaam, Tanzania) https://www.instagram.com/p/Cn8pBQWtc7M/?igshid=NGJjMDIxMWI=
0 notes
benjavibee · 5 years
Photo
Tumblr media
[Old Audio] TMK WANAUME – DAR MPAKA MORO TMK WANAUME - DAR MPAKA MORO Download Audio
0 notes